Thursday, May 18, 2006

UTUMWA ULIOKITHIRI KWENYE MASHAMBA YA MAUA- ARUSHA

Mazingira machafu ya kazi,kazi isiyo na dhamana,kazi za kulazimishwa,ubabe wa kupita kiasi kutoka kwa wamiliki wa mashamba hayo,na kuishi maisha ya samaki,ni maisha ya kawaida kwenye mashamba makubwa ya maua –kanda kazikazini,hasa Arusha (Geneve ya Africa) Wafanyakazi ndani ya mashamba haya, hufanya kazi kwa muda mrefu,hupata ujira mdogo, hudhalilishwa na kunyanyaswa kijinsia na wengine hulazimishwa kufanya mapenzi bila ridhaa yao. Hayo ndiyo maisha ya kawaida kwa wafanyakazi hawa wa mashamba ya maua.
Ukiwa nje ya mashamba haya utavutiwa sana kuyaona make yanapendeza jinsi yalivyojegengewa, kama ujawai kuyaona,utadhani ni viwanda vikubwa vikubwa vya kuzalisha Nyuklia au ni viwanda vya nguo. Ukiyasogelea utapenda kuyasogelea zaidi, ndipo utakapoona watu wakiwa ndani ya nyumba ndefu iliyotengenezwa kwa karatasi za nailoni kwa kimombo nyumba hiyo inaitwa(Green house)yaani nyumba nyeupe. Kazi ya nyumba hii ni mahali ambapo maua hupandwa ndani, utajiuliza mbona sisi maua yetu yako nje ya nyumba. Sasa maua haya hupandwa ndani ya nyumba hii (Green house)kazi ya hii nyumba hasa, ni kudhibiti na kuruhusu mwanga na hewa vinavyoitajika kwenye maua na vinginevyo. Hivyo wafanyakazi wa maua huwa ndani ya hii nyumba nao wakigombania hewa,mwanga na maua ambayo upitia au kuruhusiwa kupita kwenye Green house.
Maua haya hupigwa Dawa kali za kemikali ili wadudu wasiyashambulie maua hayo ambayo, uwekewa mbolea mbali mbali za yabisi na maji, vyote hivi hufanyika ndani ya Greenhouse au nyumba ya kijani, ambamo wafanyakazi nao huwa ndani ya nyumba hii. Ebu pata picha kwanza,uko ndani ya nyumba yenye Dirisha moja dogo nyuma umepiga sumu kuua mbu au mende, je utaweza kukaa humo ndani na kuendelea kufanya kazi zako kama kawaida. Sasa kwenye mashamba haya au nyumba hizo yaani Green house mabo huwa hivyo, Dawa hupigwa wakati wafanyakazi wakiwa ndani katika maua.Sasa kinachofanyika huwa wafanyakazi wanahama kila mpiga Dawa anapowafikia.Yaani mpiga Dawa akifika unakofanyia kazi inabidi uhamie kule alikotoka kupiga Dawa. Kumbuka hawa watu wako ndani ya nyumba ndefu Green house, sasa cha kuogopesha zaidi wakati wa mambo yote haya ya upigaji wa madawa na uchumaji wa maua wakifanyika kwa wakati mmoja wafanyakazi wa haya mashamba ufanya kazi zao bila vifaa vya kufanyia kazi. Vifaa kama glove,makisi,yaani vivaa vya kuvaa mikononi na usoni au puani.
Sasa juzi nilitembelea mashamba haya niliyoyakuta ni zaidi ya niliyokuwa nayafahamu. Kulingana na maelezo ya wafanyakazi hao. Katika kipindi cha msimu mkuu au high peek wanavyokiita wao,ambacho uwa ni kipindi cha kuanzia mwezi wa kumi mpaka mwezi wa Tatu na kipindi cha valentine (Siku ya wapendanao).Wafanyakazi hao ufanya kazi masaa,kumi na manane 18,kuanzia saa kumi na moja 11 mapambazuko mpaka saa tano usiku bila kulipwa muda wa ziada (Overtime).Mbali na kurudi usiku, Hakuna usafiri unaotolewa kwa wafanyakazi wakiwemo wanawake na wasichana ambao wamejikuta mara kwa mara kwenye hatari ya kubakwa.
Idadi kubwa ya wafanyakazi hao ni wanawake ambao ni zaidi ya asilimia sitini (60%),Hawa wamejikuta kwenye Hatari hasa ya kukosa kizazi (Watoto)kwa sababu ya madawa yanayotumika kwenye mashamba hayo. Katika uchunguzi wangu, niliweza kupata maelezo ya mshahara kima cha chini mpaka juu. Katika mashamba haya wafanyakazi ulipwa mshahara kuanzia sh 30,000 mpaka wastani wa sh 75,000 kwa mwezi, na Hakuna ongezeko la mshahara. Labda uamue kuamia kwenye shamba jingine lenye maslahi zaidi kidogo. Mbali na mshahara mdogo Hakuna marupurupu yoyote ambayo mfanyakazi huyapata.
Wanawake nilioongea nao walinieleza kuwa,wamejikuta hata wengine siku zao za Hedhi hazionekani hata kama hawana mimba, kwa sababu ya Hadhali za madawa walinieleza katika mashamba haya hakuna hata Zahanati ya kutoa huduma ya kwanza pale ambapo mfanyakazi hutadhulika na madawa hayo,mbali na kwamba watu (Wafanyakazi­)wanadhulika mara kwa mara mpaka wengine kupoteza maisha na wamiliki wa mashamba haya au Selikali .
Uzalishaji na unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake unaofanywa na wasimamizi wa mashamba haya na wakati mwingine wafanyakazi wenzao wa kiume umekithili kwenye mashamba haya. Wakati mwingine wamejikuta wakisimamishwa kazi kama wakikataa kufanya nao mapenzi. Hiki ni kitu ambacho hufanyika kila siku,Bila vyombo vya Dola kujua. Katika mashamba mengine wanawake/wasichana huficha kusema kama wana mimba ili wasije wakafukuzwa kazi kabla ya Maternity leave.Wakati mwingine wanaamua kutoa mimba pindi pale wanapogundua kuwa Baba wa mtoto hajulikani au niwakutatanisha. Hapo wasichana wanaona ni bora kutoa mimba na haya ni ya kawaida kwenye mashamba haya.
Katika Arusha mashamba haya ya maua yamekua haraka sana katika miaka 10 iliyopita yakichangia Asilimia 15 za pato la mkoa kwenye fedha za kigeni yakiwa ya Tatu nyuma ya utalii na madani. Mavuno yake, yameongezeka kwa kipindi cha miaka mitano 5 kutoka tani 15,000 mpaka tani 30,000 kwa mwaka. Yakiongeza na kuleta mamilioni ya fedha kwenye nchi. Mbali na uongezekaji yake Hakuna faida yoyote wanayoipata wafanyakazi na wananchi wanaozungukwa na mashamba hayo, matokeo yake ni utumwa mkubwa walionao. Ukiangalia mikono ya wafanyakazi hasa ya wanawake ambao ushughulika zaidi na kukata na kufunga maua,lazima utokwe na machozi. Mikono imebadilika rangi,mwingine kucha hamna,uso umebabuka,lakini cha kushangaza hata Serikali ya Kata wanamofanyia kazi imenyamaza kimya kana kwamba hawajui kinachoendelea. Ebu jiulize ingawa, Hata Baadhi ya viongozi wengine wa chama na Serikali, watoto wao wanafanya kazi kwenye mashamba hayo lakini wamekaa kimya kila mmoja akiogopa kuwa wa kwanza kulisema. Ingawa mimi nimelisema ila mimi siogopi make nimeishaamua kuingia kwenye ulingo wa mapambano ya kuwatetea wanyonge kwa kutumia kipaji changu cha kuandika nilichopewa na mwenyenzi Mungu. Ningekuwa mwanasiasa ningepitia siasa ila mimi sio mwanasiasa. Basi napitia kwenye karamu.
Cha kushangaza kabisa tena sema kwenye mashamba haya hata vyama vya wafanyakazi vimenyamaza kimya kana kwamba tatizo hili hawalijui. Wafanyakazi hawa wa mashamba hawajui haki na majukumu yao kwenye vyama vya wafanyakazi Makampuni mengine yamenda mbali hata kufikia hatua ya kuwakataza wafanyakazi wao kutoshiriki au kutokujiunga na chama chochote cha wafanyakazi cha kushangaza zaidi nikwamba zaidi ya Asilimia 80% ya wafanyakazi wa mashamba hayo, Hawana ajira ya kudumu, wengi wao wanafanya kazi kama vibarua licha ya kwamba wamefanya kazi hapo zaidi ya miaka mitano. Ingawa wafanyakazi hao wameishapeleka malalamiko yao kwa mkuu wa Mkoa tangia mwaka jana Hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali dhidi ya wamiliki hao wa mashamba.
Ndani ya mashamba hayo,kuna mambo mengi wanayofanyiwa wafanyakazi hao, kama kupigwa mpaka kufa kuachiwa mbwa wawangate wafanyakazi,madawa makali yanayopigwa kwenye mashamba yanayofikia hatua ya kuwalewesha wafanyakazi, wakati mwingine kwenda kufia majumbani mwao bila Serikali kujua.
“Ni hatari tupu na tunafanya kazi, sasa wewe Bosi niambie tunafanya nini?” Aliuliza mama mmoja niliyekutana naye akitoka kazini uku akiwa amebeba mtoto mgongoni. “Sasa nahuyu mtoto naye anaingia kwenye nyumba hii Green house?” Niliuliza. “Sasa atakaa wapi?”alijibu na haya madawa hayamdhuru? Niliuliza, akijibu “mapenzi ya Mungu ingawa sio mara kwa mara nakuja naye”.Ebu fikilia huu ni uwekezaji au ni utumwa mwingine tumewaletea wananchi wetu. Mashamba mengine huku Arusha yamezungushiwa na nyaya za umeme, Ebu fikiria watoto wakisogelea itakuwaje? Kuna sehemu nyingine wazungu hawa(Wakulima wa mashamba ya maua)walitaka kuamsha shule. Eti iko kwenye mashamba yao. Wengine wamewazuia wananchi kuchota maji kisa Eti maji yako Mashambani mwao, walichokifanya kuwahi ni kuweka uzio wa umeme. Utumwa huu mashambani umekidhili mpaka unawalazimisha wasichana wadogo wanaofanya kazi mashambani humo kutoa rushwa ya ngono. Msichana lazima atoe rushwa ya ngono. Kila siku tunasema Rushwa ya ngono maofisini nenda mkafanye research kwenye mashamba ya maua mkaone. Namalizia kwa kusema kuwa utumwa umekithiri kwenye mashamba ya maua Arusha.

2 Comments:

At 12:06 PM, Blogger Jeff Msangi said...

Ludovick,
Hii inatia uchungu sana.Nimewahi kulisikia hili siku za nyuma lakini sikuwahi kupata picha kwamba hali ni mbaya namna hii.Tunahitaji kulishughulikia mara moja.Nitakusaidia.

 
At 8:11 PM, Blogger boniphace said...

Nomba mtumie habari hii Yahya Charahani mzee wa Mshitu tazama E mail yake pale kwenye Gazeti Tndo lake na kabla ya kufanya hivyo isome kwanza na kuipanga upya ili usirdie mambo kisha yaweza kuchapwa gazetini huko nyumbani. Naomba fanya hivi maana nafahamu Jeff NAYE AMEKUWA KATIKA MKAKATI FULANI BAADA YA KUIPATA HABARI HII HAPA. Mwisho nikushukuru kwa ujasiri wako wa kuamua kuwasemea watu wadogo. Mungu atakuongezea kwa kazi hii.

 

Post a Comment

<< Home